Ushawishi wa Tanzania Duniani utategemea na Ubora wa Sera ya Mambo ya Nje inayorekebishwa .
Imeelezwa kuwa ili Tanzania iweze kufikia malengo ya Maendeleo iliyojiwekea, lazima iwe na Sera Bora ya Mambo ya Nje inayozingatia maoni na matakwa ya makundi yote ya wadau nchini.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Ikulu Zanzibar, Mhe. Ali Suleiman Ameir ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika Kongamano la wadau la kukusanya maoni kuhusu marekebisho ya Sera Mpya ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001 lililofanyika kwenye Hoteli ya Golden Tulip mjini Zanzibar tarehe 05 Februari 2024.
Kongamano hilo ambalo ni la tatu kufanyika ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kushirikisha wananchi kutoa maoni yatakayozingatiwa katika zoezi la kurekebisha Sera ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001.
Mwenye dhamana ya kusimamia Sera hiyo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba ametaja sababu za Wizara yake kuratibu makongamano hayo ambapo alisema linalofuata litafanyika Pemba tarehe 10 Februari 2024.
Alieleza kufanyika kwa makongamano hayo ni utekelezaji wa misingi ya utawala bora ambayo inasisitiza umuhimu wa kushirikisha wadau katika utungaji wa Sera za nchi, ikiwemo Sera ya Mambo ya Nje.
Alieleza pia kuwa Sera ni Tamko linalotoa mwongozo namna nchi itakavyoshughulikia ushirikiano na uhusiano wake na dunia. Hivyo, utungaji wa Tamko muhimu kama hilo lazima lishirikishe wadau wote.
Mhe. Makamba aliwambia washiriki wa Kongamano hilo kuwa Tanzania ina ushawishi mkubwa duniani tofauti na nguvu zake za kiuchumi na kijeshi kutokana na kuwa na Sera bora ya Mambo ya Nje. Hivyo, ili iendelee kuwa na ushawishi huo duniani lazima itungwe Sera imara itakayozingatia maoni ya wadau wote.
Aliendelea kueleza kuwa Sera ya Mambo ya Nje ina uhusiano wa moja kwa moja na malengo ya Maendeleo ya nchi. Hivyo, mchakato wa utungaji wa Sera ya Mambo ya Nje lazima ushirikishe wadau kwa kuwa maendeleo ni jambo linalomgusa kila mmoja.
Alihitimisha hotuba yake kwa kutaja baadhi ya mambo yaliyosababisha Serikali kufanya marekebisho ya Sera hiyo. Mambo hayo ni pamoja na mabadiliko yanayotokea duniani kama mabadiliko ya tabianchi, uvumbuzi wa teknolojia mpya, kuibuka kwa wadau wapya wa maendeleo wenye nguvu na ushawishi na Watanzania wengi hawakuwepo wakati wa utungaji wa Sera Mpya ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001.
Kongamano hilo limehudhuriwa na viongozi mbalimbali wwkiwemo Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Mhe. Idrisa Mustafa Kitwana: Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Ikulu Zanzibar, Bw. Salehe Juma Mussa, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (EAC), Balozi Stephen Mbundi, Naibu Katiibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaibu Mussa, Mabalozi wa Tanzania Nje ya Nchi, Mabolozi Wastaafu akiwemo Balozi Amina Salum Ali, viongozi wa Vyama vya Siasa, Asasi za Kiraia, Wakuu wa taasisi za Serikali na Sekta Binafsi, Wakuu wa Vyombo vya habari, wanazuoni na wananchi kwa ujumla.
High Commissioner Of The United Republic Of Tanzania To The Republic Of South Africa South Africa, H.E James G. Bwana Has Presented Copies Of His Credentials And Officially Commenced His Tour Of Duty As Per Diplomatic Practices In South Africa.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mara ya kwanza imefanya majadiliano ya kidiplomasia na Serikali ya Finland kwa lengo la kuimarisha, kukuza na kudumisha ushirikiano katika sekta mbalimbali za kipaumbele kwa maslahi ya pande zote mbili.
Pamoja na Tanzania kuwa na uhusiano mzuri na nchi za Nordic, Finland ndiyo nchi ya kwanza kufanya majadiliano ya kidiplomasia na Tanzania. Chimbuko la majadaliano hayo ni kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na nchi za Umoja wa Ulaya.
Mkutano huo kwa upande wa Tanzania umeongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) wakati upande wa Finland umeongozwa na Naibu Waziri katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Finland anayeshughulikia Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa, Mhe. Pasi Hellman.
Akizungumza katika mkutano uliokutanisha pande hizo mbili leo tarehe 14 Disemba, 2023 Jijini Dar es Salaam, Waziri Makamba amesema kuwa kutetea na kulinda misingi ya demokrasia na utawala bora ni kipaumbele cha Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Waziri Makamba ameeleza kuwa maboresho yaliyofanyika katika sheria ya vyama vya siasa na sheria ya uchaguzi yameleta mageuzi katika kuendesha chaaguzi mbalimbali nchini na uhuru wa vyama vya siasa kuendesha shughuli zake nchini.
Aidha, Tanzania itaendelea kulinda na kukuza misingi ya haki za binadamu, demokrasia na utawala bora kama nguzo muhimu ya kuleta maendeleo endelevu nchini.
Kwa upande wake, Naibu Waziri katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Finland anayeshughulikia Ushirikiaano wa Maendeleo ya Kimataifa, Mhe. Pasi Hellman amesema ushirikiano kati ya Finland na Tanzania umekuwa imara kwa zaidi ya miaka 50 na utaendelea kuimarika kutokana na misingi imara ya ushirikiano iliyopo baina ya mataifa hayo.
“Huu ni mkutano wetu wa kwanza wa majadiliano ya kidiplomasia kati ya Finland na Tanzania ambapo umelenga kuimarisha ushirikiano, kubadilishana ujuzi na uzoefu wa masuala mbalimbali yanayohusu diplomasia na maendeleo katika sekta mbalimbali baina ya nchi zetu”.
Kadhalika kupitia mkutano huo, viongozi hao pamoja na mambo mengine, wamejadili masuala ya biashara na uwekezaji, uwezeshaji kiuchumi, uwezeshaji wanawake, ushirikiano wa kikanda kati ya Ulaya na Afrika, kizazi cha usawa, hali ya hewa, mabadiliko ya tabianchi pamoja na masuala yanayohusu ulinzi na usalama.
Mkutano huo ulihudhuriwa na Makatibu Wakuu kutoka Wizara za Kisekta (Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Elimu, Uchukuzi, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Ulinzi na Makamu wa Rais Mazingira).
Wengine ni Balozi wa Tanzania Nchini Finland, Balozi wa Finland nchini Tanzania pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).
H.e amb. James g. Bwana, the high commissioner-designate of tanzania to south africa held maiden meetings with local & home based staff of tanzanian high commission in the republic of south africa. The meetings aimed at establishing bonds and setting priorities for the representational work ahead.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba (Mb) ametembelea mradi wa ujenzi wa jengo la ofisi za Wizara unaoendelea katika mjini wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Lengo la kutembelea mradi huo ni kujionea hatua iliyofikiwa katika ujenzi na kufanya mazungumzo na wasimamizi wa mradi ili kuwa baini uwepo wa changamoto zinazoweza kukwamisha ukamilishwaji wa mradi kwa wakati na viwango vinavyotarajiwa
Akizungumza na mkandarasi wakati wa ziara hiyo ya ukaguzi Mhe. Makamba amepongeza hatua iliyofikiwa na amemtaka mkandarasi wa ujenzi wa jengo hilo kuongeza kasi ili maradi huo ukamilike na kukabidhiwa kwa wakati.
“Pamoja na kazi nzuri iliyofanyika katika ujenzi wa jengo hili, bado kazi iliyobaki ni kubwa inabidi muongeze bidii zaidi ili mradi ukabidhiwe na jengo lianze kutumika na hatimaye kuleta haueni ya tatizo la uhaba wa ofisi kwa watumishi wa Wizara” amesema Mhe. Makamba
Katika ziara hiyo Mhe. Waziri Makamba aliambatana na Makatibu Wakuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samuel Shelukindo, na Balozi Stephen Mbundi anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki na watendaji wengine wa Wizara.
Jengo hilo litakalogharimu kiasi cha Shilingi bilioni 22.9 hadi kukamilika kwake lilianza kujengwa mwezi Januari 2022. Ujenzi huo unaogharamiwa na Serikali unalenga kuziwezesha Wizara na Taasisi za Serikali kuwa na majengo ya kudumu katika mji wa Serikali.
Mradi wa ujenzi wa jengo hilo unatekezwa na Umoja wa makampuni ya Sole works na mshauri elekezi ambaye ni Chuo Kikuu cha Ardhi.
Ambassador of tanzania to kenya h.e. dr. Bernard kibesse presented his letters of credence to president of the republic of kenya, h.e. williams ruto at the state house in nairobi. They reaffirmed their commitment to continue cooperating together to cement bilateral cooperation btn tanzania &kenya
Mhe. Caesar C. Waitara, Balozi wa Tanzania nchini Namibia amekutana na Mhe. Laura Veendapi McLeod-Katjirua, Gavana wa Mkoa wa Khomas, ambao ni Makao Makuu ya Namibia kwa lengo la kujitambulisha na kujadili maeneo ya ushirikiano kati ya Tanzania na Namibia
Balozi wa Tanzania nchini Algeria Mhe. Iman Njalikai amesema Chemba ya Biashara ya Algeria imedhamiria kununua kahawa na ufuta kutoka Tanzania sambamba na kuimarisha biashara baina ya Tanzania na Algeria.
Balozi Njalikai amesema hayo leo Novemba 29 2023 baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Chemba ya Biashara ya Algeria Kamel HAMENNI kwenye maonesho ya Kimataifa ya Kuchakata Taka na Kuziongezea Thamani (REVED) yanayoandaliwa na Chemba ya Biashara ya Algeria kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Utunzaji Taka, yaliyofanyika katika viwanja vya maonesho vya SAFEX, Algiers.
Amesema kuwa katika kufanikisha mipango hiyo wamekubaliana kusaidia kukamilisha mpango wa uundwaji wa Baraza la Biashara kati ya Chemba hiyo na Chemba ya Biashara ya Tanzania ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa makubaliano yaliyosainiwa wakati wa Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Algeria Agosti 2023.
Katika hatua nyingine, Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) lilitumia fursa ya maonesho hayo kuonesha namna Tanzania ilivyopiga hatua katika kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki.
“NEMC kupitia imeweza kuvutia wawekezaji kutoka Algeria kuwekeza kwenye eneo la vifungashio rafiki kwa mazingira hii itasaidia kuongeza thamani ya bidhaa zinazozalishwa nchini” Amesema Balozi Njalikai.
Kupitia maonesho hayo yaliyoanza tarehe Novemba 27, 2023 na kutarajiwa kufungwa tarehe Novemba 30, 2023, Balozi Njalikai alipata fursa ya kuona Teknolojia mbalimbali zinazotumika kuchakata na kuongeza thamani ya taka zinazozalishwa kwenye maeneo mbalimbali ya miji.